Psalms 139:1-12

Mungu Asiyeweza Kukwepwa

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 aEe Bwana, umenichunguza
na kunijua.
2 bUnajua ninapoketi na ninapoinuka;
unatambua mawazo yangu tokea mbali.
3 cUnafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu;
unaelewa njia zangu zote.
4 dKabla neno halijafika katika ulimi wangu,
wewe walijua kikamilifu, Ee Bwana.

5 eUmenizunguka nyuma na mbele;
umeweka mkono wako juu yangu.
6 fMaarifa haya ni ya ajabu mno kwangu,
ni ya juu sana kwangu kuyafikia.

7 gNiende wapi nijiepushe na Roho yako?
Niende wapi niukimbie uso wako?
8 hKama nikienda juu mbinguni, wewe uko huko;
nikifanya vilindi
Vilindi ina maana ya Kuzimu, ambayo ni Sheol kwa Kiebrania.
kuwa kitanda changu,
wewe uko huko.
9Kama nikipanda juu ya mbawa za mapambazuko,
kama nikikaa pande za mbali za bahari,
10 jhata huko mkono wako utaniongoza,
mkono wako wa kuume utanishika kwa uthabiti.

11Kama nikisema, “Hakika giza litanificha
na nuru inayonizunguka iwe usiku,”
12 khata giza halitakuwa giza kwako,
usiku utangʼaa kama mchana,
kwa kuwa giza ni kama nuru kwako.
Copyright information for SwhNEN